Trevor Tony

Saturday, May 14, 2022

Historia ya vita Kati Ya Majeshi Ya Uingereza dhidi ya majeshi ya kijerumani katikati ya nchi ya Tanganyika eneo la mto Rufiji

Tarehe 4 Januari 1917, vita ilikuwa imepamba moto. Majeshi wa Uingereza dhidi ya majeshi ya kijerumani katikati ya nchi ya Tanganyika eneo la mto Rufiji.



Askari wa kingereza, jina lake Frederick, alikuwa amejificha mahali kukabiliana na askari wa kijerumani. Akachukua "darubini" kutazama ni wapi walipo maadui. Ile anainua shingo tu, anakula risasi moja ya kichwa na kufariki papo hapo.

-------------------------

Baada ya kusikia taarifa za kuuwawa kwa Fredrick, Rais wa Marekani, bwana "Theodore Roosevelt", alihuzunika sana maana alikuwa ni rafiki yake kipenzi. Roosevelt aliandika ujumbe mzito kuonesha masikitiko ya kumpoteza rafikiye. Mwili wa askari huyo ulizikwa hapo hapo na kaburi lake lipo hadi leo hii.

Frederick, mbali na kuwa askari katika jeshi la Uingereza, alikuwa mwindaji. Alizaliwa Uingereza na kuja Afrika kwa Shughuli za upelelezi "exploration". Lakini pia kwa shughuli za uwindaji. Alikuwa mwindaji maarufu sana ulimwenguni, akianzia maeneo ya Afrika Kusini, Zimbabwe hadi Tanganyika.

"Aliua sana wanyama wetu".

Akiwa Tanganyika enzi hizo koloni la Ujerumani, Fredrick alipambana dhidi ya askari wa kijerumani katika maeneo mbalimbali ikiwemo maeneo ya kuzunguka mto Rufiji ambapo ndipo kuna pori alilokuwa akiwinda wanyama. Pori hilo lilianzishwa mwaka 1896 na serikali ya Ujerumani chini ya gavana Von Weissman. Mwaka 1905, pori hilo lilifanywa kuwa maalumu kwa shughuli za uwindaji.

Baada ya vita, Uingereza ilishinda na kutwaa koloni la Tanganyika. Na ili kumuenzi kapteni Fredrick Selous, mwaka 1922, serikali ya kikoloni ya Uingereza iliamua kugeuza pori hilo kuwa pori la hifadhi la Selous kwa kingereza "Selous Game Reserve".

Kaburi lake limo ndani ya pori hilo katika eneo la Beho-beho.

Hivyo, tumejua kwamba "hifadhi ya wanyama pori ya Selous (seluu)" imepata jina hilo kutokana na huyo Fredrick Selous.

Ahsante.
 According  to KichwaKikuu

No comments:

Post a Comment