Trevor Tony

Saturday, May 14, 2022

Picha Historia: Ya Mwalimu Nyerere ziarani Bangalore, nchini India

Hii ni picha ya kumbukumbu ipo katika kiwanda cha helikopta, Bangalore!

Inamwonesha Raisi wa kwanza wa Tanzania, Hayati Mwl. Nyerere na ujumbe wake walipotembelea India kwa ziara ya kiserikali na kufika hapo kiwandani tarehe 20 Januari, 1976.

Hindustan Aeronautics Limited (HAL) pia kinaitwa Chetak ni kiwanda ambacho bado kinaunda chopa au helikopta mpaka leo na kipo chini ya wizara ya ulinzi ya Taifa la India.
Ni jambo la furaha kuona wenzetu wameweka kumbukumbu hii nzuri!

Hakika Historia ni somo zuri sana na historia ni somo linaloishi. Na ndio maana Marcus Garvey aliwahi kusema," Watu wanaoishi bila kujua Historia na utamaduni wao ni sawa na mti usio na mizizi"

Francis Daudi


No comments:

Post a Comment